-
Nehemia 5:8, 9Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 Nikawaambia: “Kwa kadiri tulivyoweza, tumewanunua ndugu zetu wenyewe, Wayahudi, waliouzwa kwa mataifa; lakini je, sasa mtawauza ndugu zenu wenyewe,+ nasi tulazimike kuwanunua tena?” Ndipo wakanyamaza kimya, hawakuwa na lolote la kusema. 9 Kisha nikawaambia: “Jambo mnalofanya si jema. Je, hampaswi kutembea kwa kumwogopa Mungu+ wetu ili mataifa, maadui wetu, wasitushutumu?
-