-
2 Samweli 19:25-27Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
25 Alipofika* Yerusalemu kumpokea mfalme, mfalme alimuuliza: “Mefiboshethi, kwa nini hukwenda pamoja nami?” 26 Akamjibu: “Bwana wangu mfalme, mtumishi wangu+ alinidanganya. Kwa maana mimi mtumishi wako nilikuwa nimesema, ‘Acha niweke matandiko juu ya punda wangu ili nipande juu yake na kwenda pamoja na mfalme,’ kwa maana mimi mtumishi wako ni kilema.+ 27 Lakini alinichongea kwako bwana wangu mfalme.+ Hata hivyo, wewe bwana wangu mfalme ni kama malaika wa Mungu wa kweli, basi fanya jambo lolote unaloona ni jema kwako.
-