14 Basi huu ndio urithi ambao kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa koo za makabila ya Israeli waliwapa Waisraeli katika nchi ya Kanaani.+ 2 Waligawiwa urithi wao kwa kura,+ kama Yehova alivyomwagiza Musa ayagawie yale makabila tisa na nusu.+