-
1 Samweli 24:16-18Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
16 Mara tu Daudi alipomaliza kumwambia maneno hayo, Sauli akasema: “Je, hiyo ni sauti yako, Daudi mwanangu?”+ Kisha Sauli akaanza kulia kwa sauti kubwa. 17 Akamwambia Daudi: “Wewe ni mwadilifu kuliko mimi, kwa maana umenitendea mema lakini mimi nimekulipa kwa uovu.+ 18 Naam, leo umeniambia mema uliyotenda kwa kukosa kuniua Yehova aliponitia mikononi mwako.+
-