-
Luka 14:8-10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 “Mtu akikualika kwenye karamu ya ndoa, usiketi mahali pa heshima zaidi.+ Huenda pia amemwalika mtu mashuhuri kuliko wewe. 9 Naye aliyewaalika atakuja kukuambia, ‘Mwachie mtu huyu mahali ulipoketi.’ Kisha utaondoka kwa aibu na kuketi mahali pa chini kabisa. 10 Lakini unapoalikwa, nenda uketi mahali pa chini kabisa, ili mtu aliyekualika akija akuambie, ‘Rafiki yangu, nenda uketi mahali pa heshima zaidi.’ Kisha utakuwa na heshima mbele ya wageni wenzako wote.+
-