-
Mathayo 21:23-25Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
23 Baada ya kuingia hekaluni, wakuu wa makuhani na wazee wa watu wakaja alipokuwa akifundisha, wakamuuliza: “Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Na ni nani aliyekupa mamlaka hayo?”+ 24 Yesu akawajibu: “Nami nitawauliza swali. Mkinijibu basi nitawaambia ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani: 25 Ubatizo wa Yohana, ulitoka wapi? Ulitoka mbinguni au kwa wanadamu?”* Lakini wakaanza kujadiliana kati yao wakisema: “Tukisema, ‘Ulitoka mbinguni,’ atatuuliza, ‘Kwa nini hamkumwamini?’+
-