11 Kwa maana huu ndio ujumbe ambao mmesikia tangu mwanzo, kwamba tunapaswa kupendana;+ 12 si kama Kaini, aliyetokana na yule mwovu akamuua ndugu yake. Na kwa nini alimuua?+ Kwa sababu matendo yake mwenyewe yalikuwa maovu,+ lakini matendo ya ndugu yake yalikuwa ya uadilifu.+