2 Kwa maana sisi sote hujikwaa* mara nyingi.+ Ikiwa yeyote hajikwai katika neno, huyo ni mtu mkamilifu, anayeweza kuuongoza kwa lijamu mwili wake wote pia.
8 Lakini hakuna mwanadamu anayeweza kuufuga ulimi. Ulimi ni kitu kitundu chenye kudhuru, kilichojaa sumu yenye kuua.+9 Kwa ulimi tunamsifu Yehova,* aliye Baba, na bado kwa ulimi tunawalaani wanadamu ambao wameumbwa “kwa mfano wa Mungu.”+