22 Nami nikaona kwamba hakuna jambo bora kwa mwanadamu kuliko kufurahia kazi yake,+ kwa sababu hiyo ndiyo zawadi yake;* kwa maana ni nani anayeweza kumwezesha aone yatakayotukia baada ya kifo chake?+
18 Hili ndilo jambo ambalo nimeona ni jema na linafaa: kwamba mtu anapaswa kula na kunywa na kufurahia kazi yote ngumu+ anayofanya kwa jasho chini ya jua katika siku chache za maisha alizopewa na Mungu wa kweli, kwa maana hiyo ndiyo thawabu yake.*+
9 Furahia maisha pamoja na mke wako mpendwa+ sikuzote za maisha yako ya ubatili, ambazo Mungu amekupa chini ya jua, sikuzote za ubatili wako, kwa maana hilo ndilo fungu lako maishani na katika kazi yako ngumu unayofanya kwa jasho chini ya jua.+