3 Naye atafurahia kumwogopa Yehova.+
Hatahukumu kwa mambo anayoona kwa macho yake,
Wala kukaripia kulingana tu na mambo anayosikia kwa masikio yake.+
4 Atawahukumu kwa haki watu wa hali ya chini,
Na kwa unyoofu atakaripia kwa ajili ya wapole wa dunia.
Ataipiga dunia kwa fimbo ya kinywa chake+
Na kuwaua waovu kwa pumzi ya midomo yake.+