Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yoshua 23:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 “Basi sasa nakaribia kufa,* nanyi mnajua vizuri kwa mioyo yenu yote na kwa nafsi* zenu zote kwamba halikukosa kutimia hata neno moja kati ya ahadi zote nzuri ambazo Yehova Mungu wenu aliwaahidi. Zote zimetimia kwenu. Halikukosa kutimia hata neno moja aliloahidi.+

  • Isaya 55:10, 11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Kwa maana kama mvua na theluji inavyomwagika kutoka mbinguni

      Nayo hairudi huko mpaka iiloweshe dunia na kuifanya izae na kuchipuka,

      Na kumpa mbegu mpandaji na mkate yule anayekula,

      11 Hivyo ndivyo neno langu linalotoka katika kinywa changu litakavyokuwa.*+

      Halitarudi kwangu bila matokeo,+

      Bali hakika litatimiza jambo lolote linalonipendeza,*+

      Na hakika litafanikiwa katika yale ambayo nimelituma.

  • Zekaria 1:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Hata hivyo, je, maneno yangu na maagizo yangu niliyowaamuru watumishi wangu, manabii, hayakutimia kwa baba zenu?’+ Basi wakanirudia na kusema: ‘Yehova wa majeshi ametutendea kulingana na njia zetu na matendo yetu, kama alivyokusudia kututendea.’”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki