Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 31:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Nitakapowaleta katika nchi ambayo niliwaapia mababu zao+—nchi inayotiririka maziwa na asali+—nao wale na kushiba na kufanikiwa,*+ wataigeukia miungu mingine na kuiabudu na kunidharau na kulivunja agano langu.+

  • 2 Wafalme 17:13, 14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Yehova aliwaonya Waisraeli na watu wa Yuda tena na tena kupitia manabii wake wote na kila mwonaji,+ akisema: “Geukeni na kuacha njia zenu ovu!+ Shikeni amri zangu na maagizo yangu kulingana na sheria yote niliyowaamuru mababu zenu na ambayo niliwapa kupitia watumishi wangu manabii.” 14 Lakini hawakusikiliza, nao wakaendelea kuwa wakaidi kama* mababu zao ambao hawakudhihirisha imani katika Yehova Mungu wao.+

  • Nehemia 9:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 “Hata hivyo, hawakutii, bali walikuasi+ na kuigeuzia mgongo Sheria yako.* Wakawaua manabii wako waliowaonya wakurudie, nao wakatenda matendo makubwa ya ukosefu wa heshima.+

  • Isaya 1:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  4 Ole kwa taifa lenye dhambi,+

      Watu waliolemewa na dhambi,

      Uzao wa watu waovu, watoto waliopotoka!

      Wamemwacha Yehova;+

      Wamemvunjia heshima Mtakatifu wa Israeli;

      Wamemgeuzia migongo yao.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki