-
Luka 1:30-35Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
30 Basi malaika akamwambia: “Usiogope, Maria, kwa maana umepata kibali cha Mungu. 31 Tazama! utapata mimba* na kuzaa mwana+ nawe utamwita Yesu.+ 32 Huyo atakuwa mkuu+ naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Zaidi,+ na Yehova* Mungu atampa kiti cha ufalme cha Daudi baba yake,+ 33 naye atatawala akiwa Mfalme juu ya nyumba ya Yakobo milele, na Ufalme wake hautakuwa na mwisho.”+
34 Lakini Maria akamuuliza malaika: “Hilo litawezekanaje, kwa kuwa sina uhusiano wa kingono na mwanamume?”+ 35 Malaika akamjibu: “Roho takatifu itakuja juu yako,+ na nguvu za Aliye Juu Zaidi zitakufunika. Kwa hiyo yule atakayezaliwa ataitwa mtakatifu,+ Mwana wa Mungu.+
-