Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Mambo ya Nyakati 36:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Kwa hiyo akamleta mfalme wa Wakaldayo awashambulie,+ ambaye aliwaua wanaume wao vijana kwa upanga+ katika nyumba ya mahali pao patakatifu;+ hakumhurumia kijana wa kiume wala bikira, mzee wala aliye dhaifu.+ Mungu alitia kila kitu mikononi mwake.+

  • Yeremia 51:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  7 Babiloni amekuwa kikombe cha dhahabu mkononi mwa Yehova;

      Aliilewesha dunia yote.

      Mataifa yamekunywa divai yake;+

      Ndiyo sababu mataifa yameshikwa na wazimu.+

  • Ezekieli 29:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Ninampa Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni nchi ya Misri,+ naye atabeba utajiri wake na kuchukua nyara kwa wingi na kuipora; na vitu hivyo vitakuwa malipo ya jeshi lake.’

  • Danieli 5:18, 19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Ee mfalme, Mungu Aliye Juu Zaidi alimpa baba yako Nebukadneza ufalme na ukuu na heshima na fahari.+ 19 Kwa sababu ya ukuu ambao Mungu alimpa, watu wa makabila yote, mataifa, na lugha walitetemeka kwa woga mbele yake.+ Yeyote ambaye mfalme alitaka kumuua, alimuua, yeyote aliyetaka kumwacha hai, alimwacha hai, yeyote aliyetaka kumkweza, alimkweza, na yeyote aliyetaka kumwaibisha, alimwaibisha.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki