-
Isaya 20:3, 4Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Kisha Yehova akasema: “Kama mtumishi wangu Isaya alivyotembea akiwa uchi na bila viatu kwa miaka mitatu ili kuwa ishara+ na dalili dhidi ya Misri+ na dhidi ya Ethiopia,+ 4 hivyo ndivyo mfalme wa Ashuru atakavyowaongoza mateka wa Misri+ na wahamishwa wa Ethiopia, wavulana na wanaume wazee, wakiwa uchi na bila viatu na matako yakiwa wazi, uchi wa* Misri.
-
-
Yeremia 46:25, 26Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
25 “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Sasa ninamkazia fikira Amoni+ kutoka No,*+ Farao, Misri, miungu yake,+ wafalme wake—naam, Farao na wote wanaomtumaini.’+
26 “‘Nami nitawatia mikononi mwa wale wanaotaka kuwaua, mikononi mwa Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni+ na watumishi wake. Lakini baadaye watu watakaa ndani yake kama zamani,’ asema Yehova.+
-