Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yeremia 25:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Basi nikakichukua kile kikombe kutoka mkononi mwa Yehova na kuyanywesha mataifa yote ambayo Yehova alinituma kwao:+

  • Yeremia 25:22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 wafalme wote wa Tiro, wafalme wote wa Sidoni,+ na wafalme wa kisiwa kilicho baharini;

  • Yeremia 47:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  4 Kwa sababu siku inayokuja itawaangamiza Wafilisti wote;+

      Itamwangamiza kabisa kutoka Tiro+ na kutoka Sidoni+ kila msaidizi aliyebaki.

      Kwa maana Yehova atawaangamiza Wafilisti,

      Ambao wamebaki wa kisiwa cha Kaftori.*+

  • Ezekieli 26:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Niko dhidi yako, Ee Tiro, nami nitayainua mataifa mengi dhidi yako, kama vile bahari inavyoinua mawimbi yake.

  • Ezekieli 27:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 “Nawe, mwana wa binadamu, mwimbie Tiro wimbo wa huzuni,*+

  • Yoeli 3:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  4 Pia, kwa nini mnanitendea hivi,

      Enyi watu wa Tiro na Sidoni na maeneo yote ya Ufilisti?

      Je, mnanilipiza kisasi kwa sababu ya jambo fulani?

      Ikiwa mnanilipiza kisasi,

      Nitawalipiza kisasi haraka, naam, upesi.*+

  • Amosi 1:9, 10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  9 Yehova anasema hivi:

      ‘Kwa sababu ya maasi matatu ya Tiro,+ na hata manne, sitabadili uamuzi wangu,

      Kwa sababu walilitia mikononi mwa Edomu kundi lote la watu waliohamishwa,

      Na kwa sababu hawakukumbuka agano la ndugu.+

      10 Basi nitaushushia moto ukuta wa Tiro,

      Nao utateketeza kabisa minara yake yenye ngome.’+

  • Zekaria 9:3, 4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  3 Jiji la Tiro lilijijengea boma.*

      Lilirundika fedha kama mavumbi

      Na dhahabu kama mavumbi barabarani.+

       4 Tazama! Yehova atachukua mali za jiji hilo,

      Naye ataliangamiza jeshi lake baharini;+

      Na jiji hilo litateketezwa motoni.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki