-
2 Mambo ya Nyakati 36:15, 16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
15 Yehova Mungu wa mababu zao aliendelea kuwaonya kupitia wajumbe wake, aliwaonya tena na tena, kwa sababu aliwahurumia watu wake na makao yake. 16 Lakini waliendelea kuwadhihaki wajumbe wa Mungu wa kweli,+ wakadharau maneno yake+ na kuwakejeli manabii wake,+ mpaka ghadhabu ya Yehova ilipokuja dhidi ya watu wake,+ hivi kwamba hawangeweza kuponywa.
-
-
Ezekieli 9:9, 10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
9 Basi akaniambia: “Kosa la watu wa nyumba ya Israeli na Yuda ni kubwa sana, kubwa kwelikweli.+ Nchi imejaa umwagaji wa damu,+ nalo jiji limejaa ufisadi.+ Kwa maana wanasema, ‘Yehova ameiacha nchi hii, na Yehova haoni.’+ 10 Lakini mimi, jicho langu halitasikitika; wala sitawahurumia.+ Nitawaletea madhara ya njia yao juu ya kichwa chao wenyewe.”
-