-
Marko 7:6-8Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 Akawaambia: “Isaya kwa kufaa alitoa unabii kuwahusu ninyi wanafiki, kama ilivyoandikwa, ‘Watu hawa huniheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nami.+ 7 Wao huniabudu bure, kwa maana wanafundisha amri za wanadamu kuwa mafundisho.’+ 8 Mnaiacha amri ya Mungu, na kuyashika mapokeo ya wanadamu.”+
-