Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 15:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Ni nani kati ya miungu aliye kama wewe, Ee Yehova?+

      Ni nani aliye kama wewe, unayejidhihirisha mwenyewe kuwa mkuu katika utakatifu?+

      Wewe unayestahili kuogopwa kwa nyimbo za sifa, Wewe unayetenda mambo yanayostaajabisha.+

  • 2 Wafalme 19:22-24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Umemdhihaki na kumkufuru nani?+

      Umepaza sauti yako dhidi ya nani+

      Na kuinua macho yako yenye kiburi?

      Ni dhidi ya Mtakatifu wa Israeli!+

      23 Kupitia wajumbe wako+ umemdhihaki Yehova+ ukisema,

      ‘Kwa wingi wa magari yangu ya vita

      Nitapanda vilele vya milima,

      Sehemu za mbali sana za Lebanoni.

      Nitakata mierezi yake mirefu sana, miberoshi yake iliyo bora.

      Nitaingia mahali pake palipo ndani kabisa, misitu yake yenye miti mingi sana.

      24 Nitachimba visima na kunywa maji mageni;

      Nitavikausha vijito vyote vya* Misri kwa nyayo za miguu yangu.’

  • Isaya 10:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Siku hiyo watu wa Israeli waliobaki

      Na waliookoka wa nyumba ya Yakobo

      Hawatamtegemea tena yule aliyewapiga;+

      Bali watamtegemea Yehova,

      Mtakatifu wa Israeli, kwa uaminifu.

  • Ezekieli 39:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Nitalifanya jina langu takatifu lijulikane miongoni mwa watu wangu Waisraeli, nami sitaruhusu jina langu takatifu lichafuliwe tena; na mataifa yatalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova,+ Mtakatifu katika Israeli.’+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki