-
2 Wafalme 19:22-24Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
22 Umemdhihaki na kumkufuru nani?+
Umepaza sauti yako dhidi ya nani+
Na kuinua macho yako yenye kiburi?
Ni dhidi ya Mtakatifu wa Israeli!+
23 Kupitia wajumbe wako+ umemdhihaki Yehova+ ukisema,
‘Kwa wingi wa magari yangu ya vita
Nitapanda vilele vya milima,
Sehemu za mbali sana za Lebanoni.
Nitakata mierezi yake mirefu sana, miberoshi yake iliyo bora.
Nitaingia mahali pake palipo ndani kabisa, misitu yake yenye miti mingi sana.
-