52 Watawazingira na kuwafungia ndani ya majiji* yenu yote, katika nchi yenu yote, mpaka kuta zenu ndefu na zenye ngome mnazozitegemea zitakapoanguka. Naam, kwa hakika watawazingira katika majiji yenu yote, katika nchi yenu yote ambayo Yehova Mungu wenu amewapa ninyi.+
24 Tazama! Watu wamekuja na maboma ya kuzingira ili kuliteka jiji hili,+ na kwa sababu ya upanga,+ njaa kali, na ugonjwa hatari,+ hakika jiji litaanguka mikononi mwa Wakaldayo wanaolishambulia; mambo uliyosema yametimia yote, kama unavyoona sasa.