52 Watawazingira na kuwafungia ndani ya majiji* yenu yote, katika nchi yenu yote, mpaka kuta zenu ndefu na zenye ngome mnazozitegemea zitakapoanguka. Naam, kwa hakika watawazingira katika majiji yenu yote, katika nchi yenu yote ambayo Yehova Mungu wenu amewapa ninyi.+
25Katika mwaka wa tisa wa utawala wa Sedekia, katika mwezi wa kumi, siku ya kumi ya mwezi huo, Mfalme Nebukadneza+ wa Babiloni alikuja na jeshi lake lote kushambulia Yerusalemu.+ Akapiga kambi na kujenga ukuta kulizingira jiji hilo pande zote,+
4 “Kwa maana Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi kuhusu nyumba za jiji hili na kuhusu nyumba za wafalme wa Yuda ambazo zimebomolewa kwa sababu ya maboma ya kuzingira na kwa sababu ya upanga,+
4“Na wewe, mwana wa binadamu, chukua tofali na uliweke mbele yako. Uchonge jiji juu yake—Yerusalemu. 2 Lizingire na ujenge ukuta wa kulizingira,+ utengeneze boma la kulizingira,+ upige kambi kulizunguka,+ na kulizungushia mitambo ya kubomolea.+