Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 29:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  3 Nitapiga kambi pande zote dhidi yako,

      Nami nitakuzingira kwa ngome

      Na kujenga maboma dhidi yako.+

  • Yeremia 32:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 Wakati huo majeshi ya mfalme wa Babiloni yalikuwa yakizingira Yerusalemu, naye nabii Yeremia alikuwa amezuiliwa katika Ua wa Walinzi+ katika nyumba ya* mfalme wa Yuda.

  • Yeremia 32:28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 28 Basi Yehova anasema hivi: ‘Tazama, ninalitia jiji hili mikononi mwa Wakaldayo na mikononi mwa Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni, naye ataliteka.+

  • Yeremia 39:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 39 Katika mwaka wa tisa wa utawala wa Mfalme Sedekia wa Yuda, katika mwezi wa kumi, Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni alikuja Yerusalemu na jeshi lake lote, na kulizingira jiji hilo.+

  • Yeremia 52:4, 5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Katika mwaka wa tisa wa utawala wa Sedekia, katika mwezi wa kumi, siku ya kumi ya mwezi huo, Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni alikuja na jeshi lake lote kushambulia Yerusalemu. Walipiga kambi na kujenga ukuta kulizingira jiji hilo pande zote.+ 5 Nao walilizingira jiji hilo mpaka mwaka wa 11 wa utawala wa Mfalme Sedekia.

  • Ezekieli 4:1, 2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 “Na wewe, mwana wa binadamu, chukua tofali na uliweke mbele yako. Uchonge jiji juu yake—Yerusalemu. 2 Lizingire na ujenge ukuta wa kulizingira,+ utengeneze boma la kulizingira,+ upige kambi kulizunguka,+ na kulizungushia mitambo ya kubomolea.+

  • Ezekieli 21:21, 22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Kwa maana mfalme wa Babiloni amesimama ili kufanya uaguzi* kwenye njia panda, mahali ambapo zile barabara mbili zinatengana. Anaitikisa mishale. Anaomba ushauri kutoka kwa sanamu* zake; anachunguza ini. 22 Uaguzi* ulio katika mkono wake wa kulia umeelekezwa Yerusalemu, ili kuweka mitambo ya kubomolea, ili kutoa agizo la kuchinja, ili kupiga kelele za vita, kuweka kwenye malango mitambo ya kubomolea, kujenga boma la kuzingira, kujenga ukuta wa kuzingira.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki