4 Sehemu ya ukuta wa jiji ilibomolewa,+ na wanajeshi wote wakakimbia wakati wa usiku kupitia lango lililokuwa kati ya kuta mbili karibu na bustani ya mfalme, wakati Wakaldayo walipokuwa wakilizingira jiji; naye mfalme akafuata njia inayoelekea Araba.+
5 Nami nitatia mikononi mwa maadui wao utajiri wote wa jiji hili, mali zake zote, vitu vyake vyote vyenye thamani, na hazina zote za wafalme wa Yuda.+ Nao watapora vitu hivyo na kuvichukua na kuvipeleka Babiloni.+