Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yeremia 21:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 ‘Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: “Tazama, ninazigeuza dhidi yenu* silaha za vita zilizo mikononi mwenu, mnazotumia kupigana na mfalme wa Babiloni+ na Wakaldayo wanaowazingira nje ya ukuta. Nami nitawakusanya katikati ya jiji hili.

  • Yeremia 39:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 Katika mwaka wa 11 wa utawala wa Sedekia, mwezi wa nne, siku ya tisa ya mwezi huo, walibomoa sehemu ya ukuta wa jiji.+

  • Yeremia 39:4-7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Mfalme Sedekia wa Yuda na wanajeshi wote walipowaona walikimbia,+ wakatoka jijini wakati wa usiku kupitia njia ya bustani ya mfalme, kupitia lango lililokuwa kati ya kuta mbili, nao wakafuata njia inayoelekea Araba.+ 5 Lakini jeshi la Wakaldayo likawafuatia, nao wakamfikia Sedekia katika jangwa tambarare la Yeriko.+ Wakamkamata na kumleta kwa Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni kule Ribla+ katika nchi ya Hamathi,+ ambako alimhukumu. 6 Mfalme wa Babiloni akaagiza wana wa Sedekia wachinjwe mbele ya macho yake kule Ribla, na mfalme wa Babiloni akaagiza wakuu wote wa Yuda wachinjwe.+ 7 Ndipo akayapofusha macho ya Sedekia, kisha akamfunga kwa pingu za shaba ili ampeleke Babiloni.+

  • Ezekieli 33:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Mwishowe katika mwaka wa 12, mwezi wa kumi, siku ya tano ya mwezi wa uhamisho wetu, mtu aliyetoroka Yerusalemu alinijia+ na kusema: “Jiji limeangamizwa!”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki