-
2 Wafalme 25:3, 4Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Katika siku ya tisa ya mwezi wa nne njaa ilikuwa kali sana+ jijini, na watu waliokuwemo hawakuwa na chakula.+ 4 Sehemu ya ukuta wa jiji ilibomolewa,+ na wanajeshi wote wakakimbia wakati wa usiku kupitia lango lililokuwa kati ya kuta mbili karibu na bustani ya mfalme, wakati Wakaldayo walipokuwa wakilizingira jiji; naye mfalme akafuata njia inayoelekea Araba.+
-
-
Yeremia 52:6, 7Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 Katika mwezi wa nne, siku ya tisa ya mwezi huo,+ njaa ilikuwa kali sana jijini, na watu waliokuwemo hawakuwa na chakula.+ 7 Mwishowe sehemu ya ukuta wa jiji ikabomolewa, na wanajeshi wote wakakimbia kutoka jijini wakati wa usiku kupitia lango lililokuwa kati ya kuta mbili karibu na bustani ya mfalme, wakati Wakaldayo walipokuwa wakilizingira jiji; nao wakafuata njia inayoelekea Araba.+
-