-
Yeremia 39:4-7Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
4 Mfalme Sedekia wa Yuda na wanajeshi wote walipowaona walikimbia,+ wakatoka jijini wakati wa usiku kupitia njia ya bustani ya mfalme, kupitia lango lililokuwa kati ya kuta mbili, nao wakafuata njia inayoelekea Araba.+ 5 Lakini jeshi la Wakaldayo likawafuatia, nao wakamfikia Sedekia katika jangwa tambarare la Yeriko.+ Wakamkamata na kumleta kwa Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni kule Ribla+ katika nchi ya Hamathi,+ ambako alimhukumu. 6 Mfalme wa Babiloni akaagiza wana wa Sedekia wachinjwe mbele ya macho yake kule Ribla, na mfalme wa Babiloni akaagiza wakuu wote wa Yuda wachinjwe.+ 7 Ndipo akayapofusha macho ya Sedekia, kisha akamfunga kwa pingu za shaba ili ampeleke Babiloni.+
-