26 Nitakapoharibu hifadhi yenu ya* mikate,+ wanawake kumi wataoka mikate kwenye jiko moja tu na kuwapimia mikate kwa mizani;+ nanyi mtakula lakini hamtashiba.+
53 Ndipo mtakapolazimika kuwala watoto wenu* wenyewe, nyama ya wana wenu na mabinti wenu+ ambao Yehova Mungu wenu amewapa, kwa sababu ya kuzingirwa kabisa na kwa sababu ya mateso yatakayosababishwa na adui yenu.
21 Basi Mfalme Sedekia akaamuru Yeremia awekwe kifungoni katika Ua wa Walinzi,+ naye alipewa mkate wa mviringo kila siku kutoka kwenye barabara ya waokaji+ mpaka mikate yote ilipokwisha jijini.+ Na Yeremia akaendelea kukaa katika Ua wa Walinzi.
2 “Yehova anasema hivi: ‘Yule atakayebaki katika jiji hili atakufa kwa upanga, kwa njaa kali, na kwa ugonjwa hatari.+ Lakini yule atakayejisalimisha* kwa Wakaldayo ataendelea kuishi naye atapata uhai wake* kama nyara* na kuendelea kuishi.’+
16 Naye akaniambia: “Mwana wa binadamu, nitafanya chakula kikosekane* Yerusalemu,+ na kwa wasiwasi mwingi watakula mkate wao kwa kipimo,+ na kwa hofu nyingi watakunywa maji yao kwa kipimo.+
10 “‘“Kwa hiyo akina baba miongoni mwenu watawala wana wao,+ nao wana watawala baba zao, nami nitatekeleza hukumu kati yenu na kuwatawanya kila upande* wale waliobaki kati yenu.”’+
12 Theluthi yenu moja watakufa kwa ugonjwa hatari au kuangamia kwa njaa kali miongoni mwenu. Na theluthi nyingine watauawa kwa upanga kuwazunguka pande zote.+ Nami nitaitawanya theluthi ya mwisho kila upande,* nami nitauchomoa upanga ili kuwakimbiza.+