Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo ya Walawi 26:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 Nitakapoharibu hifadhi yenu ya* mikate,+ wanawake kumi wataoka mikate kwenye jiko moja tu na kuwapimia mikate kwa mizani;+ nanyi mtakula lakini hamtashiba.+

  • Kumbukumbu la Torati 28:53
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 53 Ndipo mtakapolazimika kuwala watoto wenu* wenyewe, nyama ya wana wenu na mabinti wenu+ ambao Yehova Mungu wenu amewapa, kwa sababu ya kuzingirwa kabisa na kwa sababu ya mateso yatakayosababishwa na adui yenu.

  • Yeremia 37:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Basi Mfalme Sedekia akaamuru Yeremia awekwe kifungoni katika Ua wa Walinzi,+ naye alipewa mkate wa mviringo kila siku kutoka kwenye barabara ya waokaji+ mpaka mikate yote ilipokwisha jijini.+ Na Yeremia akaendelea kukaa katika Ua wa Walinzi.

  • Yeremia 38:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 “Yehova anasema hivi: ‘Yule atakayebaki katika jiji hili atakufa kwa upanga, kwa njaa kali, na kwa ugonjwa hatari.+ Lakini yule atakayejisalimisha* kwa Wakaldayo ataendelea kuishi naye atapata uhai wake* kama nyara* na kuendelea kuishi.’+

  • Maombolezo 4:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  4 Ulimi wa mtoto anayenyonya hushikamana na kaakaa lake kwa sababu ya kiu.

      Watoto wadogo wanaombaomba mikate,+ lakini hakuna anayewapa.+

  • Ezekieli 4:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Naye akaniambia: “Mwana wa binadamu, nitafanya chakula kikosekane* Yerusalemu,+ na kwa wasiwasi mwingi watakula mkate wao kwa kipimo,+ na kwa hofu nyingi watakunywa maji yao kwa kipimo.+

  • Ezekieli 5:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 “‘“Kwa hiyo akina baba miongoni mwenu watawala wana wao,+ nao wana watawala baba zao, nami nitatekeleza hukumu kati yenu na kuwatawanya kila upande* wale waliobaki kati yenu.”’+

  • Ezekieli 5:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Theluthi yenu moja watakufa kwa ugonjwa hatari au kuangamia kwa njaa kali miongoni mwenu. Na theluthi nyingine watauawa kwa upanga kuwazunguka pande zote.+ Nami nitaitawanya theluthi ya mwisho kila upande,* nami nitauchomoa upanga ili kuwakimbiza.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki