-
Yoshua 23:6, 7Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 “Basi iweni jasiri sana mshike na kutekeleza mambo yote yaliyoandikwa katika kitabu cha Sheria+ ya Musa, msiiache kamwe na kwenda kulia wala kushoto,+ 7 na msishirikiane kamwe na mataifa haya+ yaliyobaki kati yenu. Hampaswi hata kutaja majina ya miungu yao+ wala kuapa kwa majina hayo, na hampaswi kamwe kuiabudu au kuiinamia.+
-
-
Yeremia 12:16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
16 “Na wakihakikisha kwamba wanajifunza njia za watu wangu na kuapa kwa jina langu, ‘Kwa hakika kama Yehova anavyoishi!’ kama walivyowafundisha watu wangu kuapa kwa jina la Baali, ndipo watakapojengwa miongoni mwa watu wangu.
-
-
Sefania 1:4, 5Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
4 “Nitaunyoosha mkono wangu dhidi ya watu wa Yuda
Na dhidi ya wakaaji wote wa Yerusalemu,
Nami nitafutilia mbali kutoka mahali hapa kila kitu kinachohusiana na* Baali,+
Jina la makuhani wa miungu ya kigeni pamoja na makuhani wenyewe,+
5 Na wale wanaoliinamia jeshi la mbinguni wakiwa juu ya paa,+
Na wale wanaoinama chini na kuapa kwamba watakuwa washikamanifu kwa Yehova+
Na wakati uleule wakiapa kwamba watakuwa washikamanifu kwa Malkamu;+
-