Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 4:27
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 Yehova atawatawanya miongoni mwa mataifa,+ na ni watu wachache tu kati yenu watakaookoka+ miongoni mwa mataifa ambayo Yehova atawafukuza ninyi mwende miongoni mwao.

  • Kumbukumbu la Torati 28:48
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 48 Yehova atawatuma maadui wenu wawashambulie, nanyi mtawatumikia+ mkiwa na njaa+ na kiu na uchi na mkiwa maskini kabisa.* Ataweka nira ya chuma kwenye shingo zenu mpaka atakapokuwa amewaangamiza.

  • Kumbukumbu la Torati 29:24, 25
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 wao pamoja na mataifa yote watauliza, ‘Kwa nini Yehova aliitendea hivi nchi hii?+ Ni nini kilichomfanya awake hasira kali hivi?’ 25 Kisha watasema, ‘Ni kwa sababu waliliacha agano la Yehova,+ Mungu wa mababu zao, ambalo alifanya pamoja nao alipowatoa nchini Misri.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 7:21, 22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Na nyumba hii itakuwa marundo ya magofu. Kila mtu atakayepita karibu nayo ataitazama kwa mshangao+ na kuuliza, ‘Kwa nini Yehova aliitendea hivi nchi hii na nyumba hii?’+ 22 Kisha watasema, ‘Ni kwa sababu walimwacha Yehova+ Mungu wa mababu zao, aliyewatoa nchini Misri,+ nao wakashikamana na miungu mingine, wakaiinamia na kuiabudu.+ Ndiyo sababu aliwaletea msiba huo wote.’”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki