-
2 Mambo ya Nyakati 36:15, 16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
15 Yehova Mungu wa mababu zao aliendelea kuwaonya kupitia wajumbe wake, aliwaonya tena na tena, kwa sababu aliwahurumia watu wake na makao yake. 16 Lakini waliendelea kuwadhihaki wajumbe wa Mungu wa kweli,+ wakadharau maneno yake+ na kuwakejeli manabii wake,+ mpaka ghadhabu ya Yehova ilipokuja dhidi ya watu wake,+ hivi kwamba hawangeweza kuponywa.
-
-
Yeremia 25:3, 4Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 “Tangu mwaka wa 13 wa utawala wa Yosia+ mwana wa Amoni, mfalme wa Yuda, mpaka leo hii, miaka hii 23, neno la Yehova limenijia, nami niliendelea kuwaambia tena na tena,* lakini hamkusikiliza.+ 4 Na Yehova aliwatuma kwenu watumishi wake wote manabii, aliwatuma tena na tena,* lakini hamkusikiliza, wala kutega sikio lenu ili msikie.+
-