19 Jamani maumivu yangu, maumivu yangu!
Ninahisi uchungu mwingi moyoni mwangu.
Moyo wangu unapigapiga ndani yangu.
Siwezi kunyamaza,
Kwa maana nimesikia sauti ya pembe,
King’ora cha vita.+
20 Msiba baada ya msiba umetangazwa,
Kwa maana nchi yote imeharibiwa.
Kwa ghafla, mahema yangu mwenyewe yameharibiwa,
Kwa muda mfupi, vitambaa vya mahema yangu.+