2 “Yehova ameniambia hivi: ‘Jitengenezee mikanda na nira, nawe uziweke kwenye shingo yako. 3 Kisha upeleke vitu hivyo kwa mfalme wa Edomu,+ mfalme wa Moabu,+ mfalme wa Waamoni,+ mfalme wa Tiro,+ na kwa mfalme wa Sidoni+ kwa mkono wa wajumbe waliokuja Yerusalemu kwa Mfalme Sedekia wa Yuda.