-
Yeremia 49:1, 2Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
49 Kuhusu Waamoni,+ Yehova anasema hivi:
“Je, Israeli hana wana:
Je, hana mrithi?
Kwa nini Malkamu+ amemiliki Gadi?+
Na kwa nini watu wake wanaishi katika majiji ya Israeli?”
2 “‘Kwa hiyo tazameni! siku zinakuja,’ asema Yehova,
‘Nitakapofanya king’ora cha vita kisikike* dhidi ya jiji la Raba+ la Waamoni.+
Atakuwa kilima chenye ukiwa,
Na miji yake itawashwa moto.’
‘Na Israeli atawamiliki wale walioichukua nchi yake,’+ asema Yehova.
-