Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 21:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Tangazo dhidi ya Duma:*

      Kuna mtu anayeniita kutoka Seiri:+

      “Mlinzi, kuna habari gani za usiku?

      Mlinzi, kuna habari gani za usiku?”

  • Ezekieli 25:12-14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Nchi ya Edomu imelipiza kisasi dhidi ya nyumba ya Yuda nayo imepata hatia kubwa kwa kulipiza kisasi dhidi yake;+ 13 kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Pia nitaunyoosha mkono wangu dhidi ya Edomu na kuwaangamiza wanadamu na wanyama waliomo, nami nitaifanya kuwa ukiwa.+ Kuanzia Temani mpaka Dedani, watauawa kwa upanga.+ 14 ‘Nitalipiza kisasi dhidi ya Edomu kwa mkono wa watu wangu Waisraeli.+ Watawaletea watu wa Edomu hasira yangu na ghadhabu yangu, ili wapatwe na kisasi changu mwenyewe,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”’

  • Yoeli 3:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Lakini Misri itakuwa ukiwa,+

      Na Edomu itakuwa nyika iliyo ukiwa,+

      Kwa sababu ya ukatili waliowatendea watu wa Yuda,+

      Katika nchi yao walimwaga damu isiyo na hatia.+

  • Amosi 1:11, 12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Yehova anasema hivi:

      ‘Kwa sababu ya maasi matatu ya Edomu,+ na hata manne, sitabadili uamuzi wangu,

      Kwa sababu alimfuatia kwa upanga ndugu yake mwenyewe,+

      Na kwa sababu alikataa kuonyesha rehema;

      Katika hasira yake anaendelea kuwararuararua bila huruma,

      Na bado anaendelea kuwakasirikia vikali.+

      12 Basi nitaishushia moto Temani,+

      Nao utateketeza kabisa minara ya Bosra yenye ngome.’+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki