- 
	                        
            
            Hesabu 13:26, 27Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
 - 
                            
- 
                                        
26 Walirudi kwa Musa, Haruni, na Waisraeli wote katika nyika ya Parani, huko Kadeshi.+ Wakawaletea habari Waisraeli wote na kuwaonyesha matunda ya nchi hiyo. 27 Hivi ndivyo walivyomwambia Musa: “Tuliingia katika nchi uliyotutuma, na kwa kweli inatiririka maziwa na asali,+ na haya ndiyo matunda yake.+
 
 - 
                                        
 
- 
	                        
            
            Kumbukumbu la Torati 6:10, 11Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
 - 
                            
- 
                                        
10 “Yehova Mungu wenu atakapowaleta katika nchi aliyowaapia mababu zenu Abrahamu, Isaka, na Yakobo kwamba atawapa ninyi+—majiji makubwa na yenye kupendeza ambayo hamkujenga,+ 11 nyumba zilizojaa vitu vizuri vya aina mbalimbali ambavyo hamkufanya kazi ili kuvipata, visima ambavyo hamkuchimba, na mashamba ya mizabibu na mizeituni ambayo hamkupanda—nanyi mtakapokuwa mmekula na kushiba,+
 
 - 
                                        
 
- 
	                        
            
            Kumbukumbu la Torati 8:7-9Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
 - 
                            
- 
                                        
7 Kwa maana Yehova Mungu wenu anawaleta katika nchi nzuri,+ nchi yenye vijito vya maji, mabubujiko na chemchemi zinazotiririka* katika bonde tambarare na katika eneo lenye milima, 8 nchi yenye ngano na shayiri, na mizabibu, mitini, na mikomamanga,+ nchi yenye mafuta ya zeituni na asali,+ 9 nchi ambayo haitakuwa na upungufu wa chakula na hamtakosa chochote, nchi yenye mawe yaliyo na chuma na katika milima yake mtachimba shaba.
 
 -