Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yeremia 51:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  7 Babiloni amekuwa kikombe cha dhahabu mkononi mwa Yehova;

      Aliilewesha dunia yote.

      Mataifa yamekunywa divai yake;+

      Ndiyo sababu mataifa yameshikwa na wazimu.+

  • Maombolezo 4:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Furahi na kushangilia, Ee binti ya Edomu,+ unayekaa katika nchi ya Usi.

      Lakini wewe pia utapitishiwa kikombe,+ nawe utalewa na kufunua uchi wako.+

  • Ezekieli 23:32-34
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 32 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi:

      ‘Utakunywa kikombe kipana na chenye kina cha dada yako,+

      Nawe utakuwa kitu cha kuchekwa na kudhihakiwa, na kikombe hicho kina mambo hayo kwa wingi.+

      33 Utalemewa na* ulevi na huzuni,

      Kikombe cha hofu na ukiwa,

      Kikombe cha dada yako, Samaria.

      34 Utalazimika kukinywa na kukimaliza kabisa+ na kuviguguna vigae vyake

      Kisha utayang’oa matiti yako.

      “Kwa maana mimi mwenyewe nimesema,” asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.’

  • Nahumu 3:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  7 Kila mtu atakayekuona atakukimbia+ na kusema,

      ‘Jiji la Ninawi limeangamizwa!

      Ni nani atakayelihurumia?’

      Nitakutafutia wapi wafariji?

  • Nahumu 3:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Wewe pia utalewa;+

      Utaenda mafichoni.

      Utatafuta kimbilio kutoka kwa adui.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki