Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 4:29
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 29 “Mkimtafuta Yehova Mungu wenu mkiwa huko, hakika mtampata,+ naam, mkiutafuta ushauri wake kwa moyo wenu wote na kwa nafsi* yenu yote.+

  • Kumbukumbu la Torati 30:1-4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 30 “Maneno haya yote yatakapotimia kwenu, baraka na laana ambayo nimeweka mbele yenu,+ nanyi myakumbuke*+ katika mataifa yote ambako Yehova Mungu wenu atawatawanya,+ 2 nanyi mrudi kwa Yehova Mungu wenu+ na kuisikiliza sauti yake kulingana na yote ninayowaamuru leo, ninyi na wana wenu, kwa moyo wenu wote na kwa nafsi* yenu yote,+ 3 ndipo Yehova Mungu wenu atakapowarudisha mateka wenu+ na kuwaonyesha ninyi rehema+ na kuwakusanya tena kutoka katika mataifa yote ambako Yehova Mungu wenu aliwatawanya.+ 4 Hata watu wenu wakitawanywa mpaka mwisho wa mbingu, Yehova Mungu wenu atawakusanya na kuwarudisha kutoka huko.+

  • 1 Wafalme 8:47, 48
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 47 nao warudiwe na ufahamu wakiwa katika nchi ya watu waliowachukua mateka,+ na kukurudia+ na kuomba kibali chako wakisema, ‘Tumetenda dhambi na kukosea; tumetenda uovu,’+ 48 nao wakurudie kwa moyo wao wote+ na kwa nafsi* yao yote katika nchi ya maadui wao waliowachukua mateka, nao wasali kwako kuelekea nchi yao ambayo uliwapa mababu zao na kuelekea jiji ambalo umelichagua na nyumba ambayo nimejenga kwa ajili ya jina lako,+

  • Yeremia 24:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Nami nitawapa moyo wa kunijua, kwamba mimi ni Yehova.+ Watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao,+ kwa maana watarudi kwangu kwa moyo wao wote.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki