-
Kumbukumbu la Torati 30:1-3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
30 “Maneno haya yote yatakapotimia kwenu, baraka na laana ambayo nimeweka mbele yenu,+ nanyi myakumbuke*+ katika mataifa yote ambako Yehova Mungu wenu atawatawanya,+ 2 nanyi mrudi kwa Yehova Mungu wenu+ na kuisikiliza sauti yake kulingana na yote ninayowaamuru leo, ninyi na wana wenu, kwa moyo wenu wote na kwa nafsi* yenu yote,+ 3 ndipo Yehova Mungu wenu atakapowarudisha mateka wenu+ na kuwaonyesha ninyi rehema+ na kuwakusanya tena kutoka katika mataifa yote ambako Yehova Mungu wenu aliwatawanya.+
-
-
Kumbukumbu la Torati 30:8-10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 “Kisha mtarudi na kuisikiliza sauti ya Yehova na kushika amri zake zote ninazowaamuru leo. 9 Yehova Mungu wenu atawaletea mafanikio mengi katika kazi yote ya mikono yenu,+ atawafanya muwe na watoto wengi na mifugo mingi na mazao mengi ya ardhi yenu, kwa maana Yehova atafurahia tena kuwafanikisha, kama alivyofurahia kuwafanikisha mababu zenu.+ 10 Kwa maana wakati huo mtaisikiliza sauti ya Yehova Mungu wenu na kushika amri zake na sheria zilizoandikwa katika kitabu hiki cha Sheria, nanyi mtarudi kwa Yehova Mungu wenu kwa moyo wenu wote na kwa nafsi* yenu yote.+
-
-
1 Wafalme 8:48, 49Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
48 nao wakurudie kwa moyo wao wote+ na kwa nafsi* yao yote katika nchi ya maadui wao waliowachukua mateka, nao wasali kwako kuelekea nchi yao ambayo uliwapa mababu zao na kuelekea jiji ambalo umelichagua na nyumba ambayo nimejenga kwa ajili ya jina lako,+ 49 basi usikie kutoka mbinguni, makao yako,+ sala yao na ombi lao la kutaka kibali, nawe utekeleze hukumu kwa ajili yao
-