-
2 Wafalme 24:1, 2Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
24 Katika siku za utawala wa Yehoyakimu, Mfalme Nebukadneza+ wa Babiloni alikuja kumshambulia, Yehoyakimu akawa mtumishi wake kwa miaka mitatu. Hata hivyo, alimgeuka na kumwasi. 2 Kisha Yehova akaanza kutuma makundi ya wavamizi ya Wakaldayo,+ Wasiria, Wamoabu, na Waamoni yaende kumshambulia. Aliendelea kutuma makundi hayo yawavamie watu wa Yuda ili kuwaangamiza, kulingana na neno la Yehova+ alilosema kupitia watumishi wake manabii.
-