22 Bwana wako Yehova, Mungu wako anayewatetea watu wake anasema hivi:
“Tazama! Nitakichukua kutoka mkononi mwako kile kikombe kinachofanya watu wapepesuke,+
Ile bilauri, kikombe changu cha ghadhabu;
Hutakinywa tena.+
23 Nitakitia mkononi mwa wale wanaokutesa,+
Wale waliokuambia, ‘Inama chini ili tutembee juu yako!’
Basi ukaufanya mgongo wako kama ardhi,
Kama barabara yao ya kutembea juu yake.”