-
Ezekieli 40:10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
10 Kulikuwa na vyumba vitatu vya walinzi katika kila upande wa lango la mashariki. Vyumba hivyo vitatu vilikuwa na ukubwa uleule, nazo nguzo za pembeni zilizokuwa pande zote mbili zilikuwa na ukubwa uleule.
-
-
Ezekieli 46:1, 2Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
46 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Lango la ua wa ndani linalotazama mashariki+ linapaswa kubaki likiwa limefungwa+ kwa siku sita za kazi,+ lakini siku ya Sabato na siku ya mwezi mpya linapaswa kufunguliwa. 2 Kiongozi ataingia ndani kupitia njia ya ukumbi wa lango,+ naye atasimama kando ya mwimo wa lango. Makuhani watatoa dhabihu yake nzima ya kuteketezwa na dhabihu zake za ushirika, naye atainama chini kwenye kizingiti cha lango na kutoka nje. Lakini lango linapaswa kubaki wazi mpaka jioni.
-