-
Isaya 6:1-3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 Katika mwaka ambao Mfalme Uzia alikufa,+ nilimwona Yehova akiwa ameketi kwenye kiti cha ufalme kilicho juu na kilichoinuliwa,+ na pindo za kanzu yake zilijaa hekaluni. 2 Maserafi walikuwa wamesimama juu yake; kila mmoja wao alikuwa na mabawa sita. Kila mmoja aliufunika uso wake kwa mabawa mawili na alifunika miguu yake kwa mawili, na kila mmoja wao aliruka huku na huku kwa mawili.
3 Na kila mmoja alimwambia mwenzake:
“Mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu ni Yehova wa majeshi.+
Dunia yote imejaa utukufu wake.”
-