19 Ndipo Mikaya akasema: “Basi, sikia neno la Yehova: Nilimwona Yehova akiwa ameketi kwenye kiti chake cha ufalme+ na jeshi lote la mbinguni likiwa limesimama kando yake, upande wake wa kulia na upande wake wa kushoto.+
9 “Nikaendelea kutazama mpaka viti vya ufalme vikawekwa na Mzee wa Siku+ akaketi.+ Mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji,+ na nywele za kichwa chake zilikuwa kama sufu safi. Kiti chake cha ufalme kilikuwa miali ya moto; magurudumu yake yalikuwa moto unaowaka.+