-
Ezekieli 1:15-18Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
15 Nilipoendelea kuwatazama hao viumbe hai, niliona gurudumu moja duniani kando ya kila mmoja wa hao viumbe hai wenye nyuso nne.+ 16 Magurudumu hayo na muundo wake yalionekana yaking’aa kama krisolito, na yote manne yalifanana. Na mwonekano wake na muundo wake ni kama gurudumu lililokuwa ndani ya gurudumu.* 17 Yaliposonga, yangeweza kwenda upande wowote kati ya zile pande nne bila kugeuka yalipokuwa yakienda. 18 Mizingo yake ilikuwa juu sana hivi kwamba iliogopesha, na mizingo ya magurudumu yote manne ilikuwa imejaa macho kuizunguka.+
-