-
Ezekieli 10:9-13Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
9 Nilipokuwa nikitazama, niliona magurudumu manne kando ya makerubi, gurudumu moja kando ya kila kerubi, na magurudumu hayo yalionekana yaking’aa kama jiwe la krisolito.+ 10 Kuhusu mwonekano wake, yote manne yalifanana, yalionekana kama gurudumu moja likiwa katikati ya gurudumu lingine. 11 Yaliposonga, yaliweza kwenda upande wowote kati ya zile pande nne bila kugeuka, kwa maana yalikuwa yakienda upande ambao kichwa kilitazama nayo yalienda bila kugeuka. 12 Miili yao yote, migongo yao, mikono yao, mabawa yao, na yale magurudumu, magurudumu ya wote wanne, yalijaa macho kila mahali.+ 13 Kuhusu yale magurudumu, nilisikia sauti ikiyaita, “Magurudumu yanayozunguka!”
-