15 Kisha nabii Yeremia akamwambia nabii Hanania:+ “Tafadhali, sikiliza, ewe Hanania! Yehova hakukutuma wewe, bali umewafanya watu hawa wautumaini uwongo.+ 16 Kwa hiyo Yehova anasema hivi: ‘Tazama! Ninakuondoa katika uso wa nchi. Utakufa mwaka huu, kwa maana umewachochea watu wamwasi Yehova.’”+