Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 32:11, 12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Ndipo Musa akamsihi* Yehova Mungu wake+ akisema: “Ee Yehova, kwa nini uwaelekezee watu wako hasira yako inayowaka, baada ya kuwatoa katika nchi ya Misri kwa nguvu kuu na kwa mkono wenye nguvu?+ 12 Kwa nini Wamisri waseme, ‘Alikuwa na nia ovu alipowatoa Misri. Alitaka kuwaua milimani na kuwaangamiza kabisa kutoka duniani’?+ Acha hasira yako inayowaka na ufikirie upya* uamuzi wako wa kuwaletea watu wako msiba huu.

  • Yoshua 2:9, 10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Akawaambia: “Najua kwamba Yehova atawapa nchi hii+ na tumeshikwa na hofu kwa sababu yenu.+ Wakaaji wote wa nchi wamevunjika moyo kwa sababu yenu,+ 10 kwa maana tumesikia jinsi Yehova alivyoyakausha maji ya Bahari Nyekundu* mbele yenu mlipotoka Misri+ na mambo mliyowatendea wale wafalme wawili wa Waamori, yaani, Sihoni+ na Ogu,+ waliokuwa ng’ambo ya* Yordani, mliowaangamiza kabisa.

  • Yoshua 9:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Wakaaji wa Gibeoni+ walisikia pia mambo ambayo Yoshua alitenda katika jiji la Yeriko+ na Ai.+

  • Yoshua 9:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Wakamjibu: “Sisi watumishi wako tumetoka nchi ya mbali sana+ kwa sababu ya heshima ya jina la Yehova Mungu wako, kwa kuwa tumesikia umaarufu wake na mambo yote aliyotenda Misri+

  • 1 Samweli 4:7, 8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Wafilisti wakaogopa, kwa sababu walisema: “Mungu amekuja kambini!”+ Basi wakasema: “Ole wetu, kwa maana jambo kama hili halijawahi kamwe kutokea! 8 Ole wetu! Ni nani atakayetuokoa kutoka katika mkono wa Mungu huyu mkuu? Huyu ndiye Mungu aliyewachinja Wamisri kwa kila aina ya mapigo nyikani.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki