-
Yeremia 43:11-13Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
11 Naye ataingia na kuipiga nchi ya Misri.+ Yeyote aliyekusudiwa kufa kwa ugonjwa hatari atakufa kwa ugonjwa hatari, na yeyote aliyekusudiwa kwenda utekwani ataenda utekwani, na yeyote aliyekusudiwa kufa kwa upanga atakufa kwa upanga.+ 12 Nami nitaziwasha moto nyumba za* miungu ya Misri,+ naye ataiteketeza na kuichukua mateka. Atajifunika kwa nchi ya Misri kama mchungaji anavyojifunika kwa vazi lake, naye ataondoka huko kwa amani.* 13 Naye atazivunja vipandevipande nguzo za* Beth-shemeshi* katika nchi ya Misri, naye ataziteketeza kwa moto nyumba za* miungu ya Misri.”’”
-