Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yeremia 23:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 “Ole wao wachungaji wanaowaangamiza na kuwatawanya kondoo wa malisho yangu!” asema Yehova.+

  • Mika 3:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Nilisema: “Sikieni, tafadhali, enyi viongozi wa Yakobo

      Nanyi makamanda wa nyumba ya Israeli.+

      Je, hampaswi kujua jambo lililo la haki?

  • Mika 3:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Viongozi* wake huhukumu ili wapate rushwa,+

      Makuhani wake hufundisha ili wapate malipo,+

      Na manabii wake hufanya uaguzi* ili wapate pesa.*+

      Na bado wanamwegemea Yehova,* wakisema:

      “Je, Yehova hayuko pamoja nasi?+

      Hakuna msiba utakaotupata.”+

  • Sefania 3:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  3 Wakuu wake walio ndani yake ni simba wanaonguruma.+

      Waamuzi wake ni mbwamwitu wakati wa usiku;

      Hawaachi hata mfupa mmoja wa kuguguna mpaka asubuhi.

  • Zekaria 11:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Ole wake mchungaji wangu asiyefaa,+ anayeliacha kundi!+

      Upanga utakata mkono wake na jicho lake la kulia.

      Mkono wake utapooza kabisa,

      Na jicho lake la kulia litapofuka* kabisa.”

  • Mathayo 23:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 “Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! kwa sababu mnawafungia watu Ufalme wa mbinguni; kwa maana ninyi wenyewe hamwingii, na mnawazuia wale wanaotaka kuingia.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki