-
Danieli 4:31-35Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
31 Mfalme alipokuwa akiendelea kusema maneno hayo, sauti ikasema hivi kutoka mbinguni: “Unaambiwa hivi, Ee Mfalme Nebukadneza, ‘Ufalme umekuponyoka,+ 32 nawe unafukuzwa mbali kutoka kati ya wanadamu. Utaishi na wanyama wa mwituni, nawe utapewa majani ule kama ng’ombe dume, na nyakati saba zitapita, mpaka utakapojua kwamba Aliye Juu Zaidi ni Mtawala katika ufalme wa wanadamu na yeye humpa ufalme huo yeyote anayetaka kumpa.’”+
33 Papo hapo, maneno hayo yakatimia kwa Nebukadneza. Akafukuzwa mbali kutoka kati ya wanadamu, akaanza kula majani kama ng’ombe dume, na mwili wake ukalowa kwa umande wa mbinguni, mpaka nywele zake zikawa ndefu kama manyoya ya tai na kucha zake zikawa kama kucha za ndege.+
34 “Mwishoni mwa kipindi hicho,+ mimi, Nebukadneza, nilitazama juu mbinguni, na ufahamu wangu ukanirudia; nami nikamsifu Aliye Juu Zaidi, nikamsifu na kumtukuza Yeye anayeishi milele, kwa sababu utawala wake ni utawala wa milele na ufalme wake ni wa kizazi baada ya kizazi.+ 35 Wakaaji wote wa dunia wanaonwa kuwa si kitu, naye hufanya kulingana na mapenzi yake mwenyewe miongoni mwa jeshi la mbinguni na wakaaji wa dunia. Na hakuna yeyote anayeweza kumzuia*+ au kumuuliza, ‘Umefanya nini?’+
-